KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, March 30, 2015

TAIFA STARS YALAZIMISHWA SARE NA MALAWI


MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, anayecheza soka ya kulipwa katika klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC), Mbwana Samatta, jana aliinusuru timu ya Taifa, Taifa Stars isiadhiriwe na Malawi.

Mbwana aliinusuru Taifa Stars baada ya kuifungia bao la kusawazisha ilipomenyana na Malawi katika mechi ya kirafiki ya kimataifa iliyochezwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza.

Katika mechi hiyo, iliyoko kwenye kalenda ya Shirikisho la Soka la Dunia (FIFA), timu hizo mbili zilifungana bao 1-1.

Mbwana aliifungia Taifa Stars bao hilo la kusawazisha dakika ya 76, akiwa katikati ya mabeki wa Malawi, baada ya kupokea pasi maridhawa kutoka kwa Mrisho Ngasa.

Malawi ilikuwa ya kwanza kupata bao dakika ya tatu ya mchezo, lililofungwa na Esau Kanyenda baada ya beki mmoja wa Taifa Stars kupangua vibaya mpira wa kona uliopigwa a Haray Nyirenda.
 
Wamalawi walitawala sehemu kubwa ya kipindi cha kwanza cha pambano hilo, ambapo wachezaji wa Taifa Stars walishindwa kuipenya ngome ya wapinzani wao.

Taifa Stars: Mwadini Ali, Shomary Kapombe, Oscar Joshua, Aggrey Morris,

Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Erasto Nyoni, Mwinyi Kazimoto, Haroun Chanongo/Mrisho Ngassa, Amri Kiemba/Salum Abubakar ‘Sure Boy’ , Thomas Ulimwengu/John Bocco na Mbwana Samatta.

No comments:

Post a Comment