KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, March 1, 2015

SIMBA YANGURUMA DAR, YAITANDIKA PRISONS 5-0






SIMBA jana ilizinduka na kutoa onyo kwa timu zinazoshiriki kwenye michuano ya ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya kuibugiza Prisons mabao 5-0 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Licha ya kuibuka na ushindi huo mnono, Simba imebaki kwenye nafasi ya nne katika msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 23 baada ya kucheza mechi 16.

Yanga inaongoza ligi hiyo kwa kuwa na pointi 31, ikifuatiwa na Azam yenye pointi 27 na Kagera Sugar yenye  pointi 24.

Katika mchezo huo ulioshuhudiwa na watazamaji wachache, Simba ilikwenda mapumziko ikiwa mbele kwa mabao 3-0. Mabao yote hayo yalifungwa na mshambuliaji chipukizi Ibrahim Hajibu.

Mabao mengine ya Simba yalifungwa na Emmanuel Okwi na Ramadhani Singano 'Messi'.

No comments:

Post a Comment