KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, August 14, 2017

OKWI AONGEZA RAHA SIMBA



MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Uganda, Emmanuel Okwi, ameongeza furaha kwa mashabiki wa klabu hiyo baada ya kuifungia bao pekee na la ushindi dhidi ya Mtibwa Sugar.

Mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, ilikuwa ya kujipima nguvu kwa timu zote mbili kwa ajili ya msimu huu wa michuano ya ligi kuu ya Tanzania Bara.

Ushindi huo ni wa pili mfululizo kwa Kocha Joseph Omog kutoka Cameroon, baada ya Jumanne iliyopita, kuwalaza mabingwa wa Ligi ya Rwanda,
Rayon Sport idadi hiyo ya bao kwenye uwanja huo.

Okwi alifunga bao hilo la pekee na ushindi dakika ya 44 baada ya kumalizia pasi kutoka kwa John Bocco.

Katika mechi hiyo, Mtibwa Sugar ilipata pigo dakika ya 30 baada ya kipa wake namba moja, Shabani Kado kuumia na nafasi yake kuchukuliwa na Abdalla Makangana.

No comments:

Post a Comment