KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, August 14, 2017

YANGA YAPIGWA 1-0 NA RUVU SHOOTING


MABINGWA watetezi Yanga wamepigwa bao 1-0 na Ruvu Shooting katika mechi ya kirafiki iliyochezwa kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

Bao pekee la Ruvu Shooting lilitokana na uzembe wa beki Abdalla Haji 'Ninja' wa Yanga, kujifunga wakati akiwa katika harakati za kuokoa mpira kwenye lango la timu yake.

Mpira uliozaa bao hilo ulitokana na krosi iliyopigwa na Shalla Juma wa Ruvu Shooting, ambapo wakati Ninja akijaribu kuiokoa kwa kichwa, mpira ulielekea langoni na kumpita kipa Ramadhani Kabwili.

No comments:

Post a Comment