KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, August 14, 2017

AJIBU AFUNGUA AKAUNTI YA MABAO YANGA



MSHAMBULIAJI mpya wa Yanga, Ibrahim Hajib, jana, alifunga bao lake la kwanza wakati timu yake hiyo ikiichapa Mlandege ya Zanzibar mabao 2-0 katika mchezo wa kirafiki uliochezwa kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar.

Ajibu, aliyesajiliwa na Yanga msimu huu akitokea Simba, alifunga bao hilo dakika ya 50, akimalizia krosi safi kutoka kwa Donald Ngoma.

Ajibu pia alitoa pasi iliyozaa bao la pili lililofungwa na Emmanuel Martin dakika ya 73.

Katika mechi hiyo, Kocha George Lwandamina wa Yanga, aliwabadilisha wachezaji wote kipindi cha pili, isipokuwa kipa Kabwili. Mabadiliko hayo ndiyo yaliyozaa mabao hayo mawili.

No comments:

Post a Comment