KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, August 26, 2017

RAIS WA FIFA AMPONGEZA KARIA, AMWALIKA ZURICH

Rais wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Gianni Infantino, ametuma salamu za pongezi kwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, Wallace Karia kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa TFF kwa kipindi cha miaka minne ijayo ya 2017-2021.


Rais Infantino katika barua yake ya Agosti 14, 2017 aliyoiandika kutoka Zurich, amesema: “Ningependa kuchukua nafasi hii kukupa pongezi zangu dhati. Nakutakia kila la kheri katika majukumu yako.”


Rais wa FIFA amesema kwamba hana shaka na uwezo wa Karia hasa ikizingatiwa kuwa alikuwa Makamu wa Rais wa kipindi kilichopita, hivyo atakuwa fursa thabiti ya kuiletea nchi maendeleo ya mchezo soka.


“Kwa wakati wote, nakuhakikishia ushirikiano wa kutosha kutoka FIFA katika malengo yako. Milango ya FIFA iko wazi wakati wowote wewe kuja kujadili masuala ya mchezo wa mpira wa miguu hasa eneo la utawala.


“Ningependa kuchukua nafasi hii kukualika kuja hapa Zurich wakati wowote kuanzia sasa ambako nitapata  fursa ya kukutambulisha maeneo mbalimbali ya FIFA. Nimeagiza upande wa utawala kuwasiliana nawe kuona na kupanga tarehe rasmi ya safari,” amesema na kuongeza:
 
“Nikutakie tena kheri na fanaka, nguvu na kila aina ya mafanikio katika majukumu yako mapya huku nikitarajia ujio wa kuonana nawe haraka.”


Wakati huo huo, Shirikisho la Mpira wa Miguu la Rwanda (FERWAFA) nalo kwa upande wake wamempongeza Rais wa TFF, Wallace Karia kwa kuchaguliwa kuwa kiongozi mpya wa shirikisho.


Katika barua ya FERWAFA iliyosainiwa na Rais wa shirikisho hilo, Nzamwita Vincent imesema kwamba Rwanda itaendelea kuwa bega kwa bega na Tanzania katika maendeleo ya mpira wa miguu kwa ushirikiano baina ya nchi mbili kadhalika ukanda wa Afrika Mashariki unaounda Baraza la Sola la nchi za Afrika Mashariki.

No comments:

Post a Comment