KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, August 15, 2017

VIONGOZI WA VILABU VYA LIGI DARAJA LA KWANZA KUFANYA KIKAO AGOSTI 18,2017

Viongozi wa Klabu zinazoshiriki Ligi Daraja la Kwanza (FDL), wanatarajiwa kuwa na kikao na uongozi wa Bodi ya Ligi (TPLB), kitakachofanyika Ijumaa Agosti 18, 2017 kuanzia saa 3.00 asubuhi kwenye Hosteli za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Pamoja na mambo mengine, kikao hicho kitakuwa maalumu kwa ajili ya kujadili Ligi Daraja la Kwanza lakini pia kutoa semina kwa viongozi hao kuhusu Leseni za Klabu (Club License).

TFF inatoa wito kwa viongozi wa juu wa klabu kuhudhuria kikao hicho muhimu . TFF ingependa kusisitiza kuzingatia muda wa kuanza kikao.

No comments:

Post a Comment