KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, August 28, 2017

SIMBA YAANZA LIGI KUU KWA KISHINDO, YAIBAMIZA RUVU SHOOTING 7-0



SIMBA imeanza michuano ya soka ya ligi kuu ya Tanzania Bara kwa kishindo baada ya kuibamiza Ruvu Shooting mabao 7-0.

Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam, mshambuliaji wa kimataifa wa Uganda, Emmanuel Okwi aliibuka shujaa wa Simba baada ya kuifungia mabao manne kati ya saba.

Kutokana na kufunga idadi hiyo ya mabao, Okwi alizaliwadiwa mpira uliotumika katika mechi hiyo baada ya pambano kumalizika.

Mabao mengine ya Simba yalifungwa na Shiza Kichuya, Juma Luizio na Erasto Nyoni.

Katika mechi nyingine za ligi hiyo, Azam iliichapa Ndanda bao 1-0 kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara, Mwadui ilishinda 2-1 dhidi ya Singida United kwenye Uwanja wa Mwadui Complex, Shinyanga wakati Mtibwa Sugar wameilaza Stand United 1-0 kwenye Uwanja wa Manungu, Turiani, Morogoro.

Timu machachari ya Mbao FC nayo iliibuka na ushindi ugenini baada ya kuichapa Kagera Sugar 1-0 kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba, Tanzania Prisons iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Mji Njombe wakati Mbeya City iliilaza Majimaji ya Songea 1-0 katika mchezo uliofanyika Uwanja wa Sokoine, mjini Mbeya.

No comments:

Post a Comment