KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, August 30, 2017

KIKAO CHA KAMATI YA TIBA KUFANYIKA LEO


Mwenyekiti wa Kamati ya Tiba ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Dkt. Paul Marealle ameitisha kikao cha Kamati ya Tiba kitakachofanyika kesho Jumatano Agosti 30, mwaka huu kuanzia saa 4:00 asubuhi.

Kikao hicho kitakachofanyika Ukumbi wa Ofisi za Makao Makuu TFF, yaliyoko Uwanja wa Kumbukumbu ya Uwanja wa Karume, Ilala jijini Dar es Salaam kitarejea shughuli zake kwa mujibu wa Katiba ya TFF sambamba na Kanuni zinazoongoza mashindano mbalimbali ya TFF.

Katika kikao hicho, pia kamati itapitia fomu za afya za utimamu wa mwili za wachezaji wote wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL); Ligi Daraja la Kwanza (FDL) na Ligi Daraja la Pili (SDL).

Miongoni mwa majukumu ya kamati hiyo ni kupitisha wachezaji wanaopaswa kucheza/kushiriki katika ligi baada ya kujirisha juu ya utimamu wa mwili wa wachezaji kwa michuano tajwa hapo juu.

No comments:

Post a Comment