KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, August 28, 2017

YANGA YABANWA MBAVU NA LIPULI


MABINGWA watetezi wa ligi kuu ya Tanzania Bara, Yanga jana waliianza vibaya ligi hiyo baada ya kulazimishwa sareya bao 1-1 na Lipuli.

Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam, Lipuli inayofundishwa na mchezaji wa zamani wa Simba, Selemani Matola, ilikuwa ya kwanza kupata bao kupitia kwa Seif Abdalla dakika ya 44.

Yanga ilisawazisha dakika moja baadaye kwa bao lililofungwa na Donaldo Ngoma, kufuatia mpira wa kona uliopigwa na beki Juma Abdul.

Lipuli ililazimika kumaliza mchezo huo ikiwa na wachezaji 10, baada ya nahodha wake, Asante Kwasi kutolewa nje kwa kadi nyekundu. Awali, alikuwa ameonyeshwa kadi ya njano.

No comments:

Post a Comment