KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, August 14, 2017

KARIA RAIS MPYA TFF, WAMBURA MAKAMU WAKE


WAJUMBE wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), wamemchagua Wallace Karia kuwa mwenyekiti mpya wa shirikisho hilo.

Katika uongozi uliopita, Karia alikuwa makamu wa rais chini ya Jamal Malinzi, anayekabiliwa na kesi ya utakatishaji fedha.

Karia alishinda wadhifa huo baada ya kuwabwaga Ally Mayay, Frederick Mwakalebela, Imani Madeha, Shija Richard na Emmanuel Kimbe.

Katika uchaguzi huo uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita kwenye ukumbi wa St. Gasper, Dodoma, Michael Wambura alichaguliwa kuwa makamu wa rais.

Wambura, ambaye aliwahi kuwa katibu mkuu wa kilichokuwa Chama cha Soka nchini (FAT) na pia klabu ya Simba, aliwabwaga Mulamu Nghambi, Mtemi Ramadhani, Robert Selasela na Stephen Mwakibolwa.

No comments:

Post a Comment