KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, August 3, 2017

SEMINA YA MADAKTARI WA TIMU ZA LIGI KUU BARA

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imeita semina ya siku moja kwa Madaktari wa timu za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara itakayofanyika Ijumaa Agosti 4, mwaka huu kuanzia saa 2.00 asubuhi kwenye Ukumbi wa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Kanuni ya 73 ya Ligi Kuu, kila klabu ya Ligi Kuu inatakiwa kuwa na daktari wa timu ambaye pamoja na mambo mengine atahakiki afya za wachezaji na viongozi wa timu.

Kila klabu inatakiwa kuhakikisha daktari wake anahudhuria semina hii muhimu itakayoendeshwa na Kamati ya Tiba ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), chini ya Mwenyekiti wake Dkt. Paul Marealle.

Bodi ya Ligi itagharamia nauli ya basi ya kuja na kurudi Dar es Salaam kwa kila mshiriki. Tunawatakia kila la kheri katika maandalizi ya ushiriki wa semina hiyo ambayo ni sehemu ya maandalizi ya Ligi Kuu ya Vodacom kwa msimu wa 2017/2018.



 

No comments:

Post a Comment