KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, August 20, 2017

WANACHAMA COASTAL UNION WAZIKA TOFAUTI ZAO



KLABU ya Coastal Union ya Jijini Tanga, imezika tofauti walizokuwa nazo awali zilizosababisha timu hiyo ishuke kutoka Ligi kuu ya Tanzania Bara msimu wa mwaka 2014/ 2015, na sasa timu hiyo imeunda umoja wa viongozi utakaokuwa na lengo la kuirejesha Ligi Kuu msimu ujao.

Akizungumza jana kwenye mkutano wa wanachama uliofanyika makaomakuu ya klabuhiyo barabara ya 11 Jijini hapa, Mwenyekiti wa kamati ya mashindano, Ahmed Hilal ‘Aurora’ alisema kutokana na kikao kilichofanyika katika hoteli ya Mkonge, kimezika tofauti hizo na sasa wapo pamoja.

Alisema miongoni mwa watu waliohudhuria mkutano huo uliorudisha umoja ni pamojana Nassor Binslum ambaye ataisaidia tena kalbu hiyo pamoja na watu wengine ili kuhakikisha timu hiyo itakayoshiriki Ligi Daraja la kwanza iweze kurejea Ligi Kuu.

“Mkutano uliofanyika Mkonge Hoteli umezika yote yaliyotokea na tumeunda umoja ambao umewezesha timue yetu kusajili wachezaji watakaokuwa na uwezo wa kupanda daraja…Tunachotaka sasa watu wote wajali Coastal kwanza mambo mengine baadaye,” alisema Aurora.

Coastal iliteremka daraja baada ya viongozi kuhitafiliana na  Aurora akiwa Mwenyekiti aliyeipandisha daraja timu hiyo msimu wa 2011-2012 alijiuzulu wadhifa huo na baadaye timu kufanya uchaguzi uliomweka madarakani Dkt Ahmed Twaha ambaye aliishusha daraja akiwa na katibu wake Kassim El-Siagi na Akida Machai.

Mgogoro huo ulisababisha baadhi ya watu kwenda kujiunga na timu ya Mgambo JKT ambayo nayo ilishuka daraja hadi la kwanza huku wanachama wengine wakienda katika timu hiyo ambapo zote mwaja jana zilizoposhiriki ligi daraja la kwanza hazikufanya vizuri.

“Tumesamuheana kabisa na sasa tupo pamoja, tusianze kunyoosheana vidole na kufukua makaburi yaliyipita hatutafika tunapotaka kwenda lakini lazima mkumbuke mpira sasa ni fedha…Nawakumbusha pia lipeni ada zenu muwe na sauti kwa viongozi hawa,” alisema Aurora.

Makamu Mwenyekiti wa timu hiyo Mohamed Musni, alisema kwamba hivisasa uongozi wa klabu hiyo umepanga kuhakikisha inafanya vizuri katika Ligi daraja la kwanza itakayoanzamwezi ujao ili wawqeze kurejea kwa kishindo Ligi Kuu.

Mjumbe wa kamati ya utendaji ya timu hiyo Abdallah Zuberi ‘Unenge’, aliwataka wanachama kuhakikisha wanaacha majungu ya kupeleka habari zitakazowarudisha kule walipotoka na badala yake wahubiri umoja kwa faida ya timu hiyo.

Kaimu Katibu Mkuu Nassoro Kibabedi, aliwataka wanachama waisaidie timu hiyo katika kipindi hiki na kamwe wasibweteke wakiamini kwamba wafadhili watafanya kila kitu hivyo walipeada zao ili ziweze kuisaidia klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment