KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, August 20, 2017

YANGA YAMALIZA KAMBI PEMBA KWA USHINDI


Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara Yanga wamemaliza Kambi yao Visiwani Pemba kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Jamhuri mchezo wa kirafiki wa kujiandaa na msimu pamoja na Mechi ya Ngao ya Hisani utakaowakutanisha na mahasimu wao Simba Agosti 23 mwaka huu kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Wakicheza katika uwanja wa Gombani uliopo visiwani humo Yanga walipata bao hilo kupitia kwa beki wao wa kushoto,Mwinyi Hajji kwa shuti kali lililoenda moja kwa moja na unakuwa ushindi wa tatu wakiwa Zanzibara na ukiwa wa pili visiwani Pemba baada ya Jumatano kuwafunga timu ya Chipukizi bao 1-0 ambalo lilifungwa na Ibrahim Ajibu.

Baada ya hapo walipita visiwani Unguja na kucheza na Mlandege na kupata ushindi wa jumla ya mabao 2-0 yakifungwa na Ibrahimu Ajibu na Emmanuel Martin huku kocha Mkuu George Lwandamina akianza na vikosi viwili kipindi cha kwanza kilikuwa hiki Kabwili, Juma Abdul, Mwinyi Mngwali, Abdallah Hajji ‘Ninja’, Nadir Haroub ‘Cannavaro’/Pato Ngonyani dk34, Maka Edward, Pius Buswita, Said Juma ‘Makapu’, Amissi Tambwe/Said Mussa dk34, Matheo Anthony na Juma Mahadhi/Yussuf Mhilu dk34.

Kipindi cha pili Yanga walifanya mabadiliko kwa kukitoa kikosi kizima na kuingiza hiki Youthe Rostand, Hassan Kessy/Juma Abdul dk70, Gardiel Michael, Kevin Yondan, Andrew Vincent ‘Dante’, Papy Kabamba Tshisbimbi, Thabani Kamusoko, Donald Ngoma, Ibrahim Hajib, Emmanuel Martin na Raphael Daudi.

Hata hivyo hakikuweza kubadili matokeo na kubaki kuwa bao moja hilo na kujiweka mguu sawa kuwavaa watani wao wa Jadi Simba kwenye ngao ya hisani Mchezo unaotarajiwa kuwa na upinzani Mkubwa hii inatokana na usajili uliofanywa na timu hizo.

Yanga wanatarajia kuingia jijini Dar es salaam Siku ya Jumanne ya wiki inayoanza kesho tayari kwa vita ya Ngao ya Hisani pamoja na kuanza Mikikimikiki ya Ligi Kuu ya Tanzania bara linalotanzamiwa kufunguliwa Agosti 26 huku Mabingwa hao watetezi wakitaraajia kutupa karata yao siku ya Jumapili ya Agosti 27 kuvaana na wageni wa Ligi timu ya Lipuli FC kutoka Iringa.

No comments:

Post a Comment