KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, August 15, 2017

SEMINA YA WANACHAMA WA SIMBA KUELEKEA KWENYE MFUMO WA HISA KUFANYIKA KESHO


SIMBA SPORTS CLUB
DAR ES SALAAM
15-8-2017
            TAARIFA KWA UMMA

Klabu ya Simba kesho inatarajiwa kufanya Semina kubwa ya Wanachama wote wa klabu hiyo.
Semina hiyo inalenga kujenga uelewa mpana zaid juu ya muundo mpya wa klabu, uliotokana na mabadiliko ya katiba yaliyofanywa na wanachama hao,na kusajiliwa na Msajili wa Vilabu nchini.
Maandalizi yote ya Semina hiyo yamekamilika,na itafanyika kesho tarehe 16-8-2017,Jumatano Saa Nane na Nusu mchana(8.30) na itafanyikia kwenye ukumbi wa Mikumi uliopo kwenye eneo la maonyesho ya kimataifa ya biashara ya Sabasaba (PTA) kurasini hapa jijini Dar es salaam.
Tunawaomba wanachama wote popote walipo waje kwa wingi hapo kesho, huku klabu ikiwaomba viongozi wa Simba Wilaya ya Temeke waandae utaratibu mzuri wa kuwapokea wageni.
IMETOLEWA NA….
HAJI S MANARA
MKUU WA HABARI SIMBA SC
SIMBA NGUVU MOJA

No comments:

Post a Comment