KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, August 3, 2017

YANGA, SINGIDA UNITED SASA KUKIPIGA JUMAMOSI


Ile mechi ya kirafiki ya Yanga na Singida United iliyopangwa kuchezwa Agosti 6 imerudishwa siku moja ili kupisha shughuli za kiserikali.

Rasmi mchezo huo utapigwa Agosti 5 kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar Es Salaam ikiwa ni pamoja na utambulisho wa wachezaji wapya waliosajiliwa msimu huu tayari kwa mikikimikiki ya Ligi kuu Tanzania Bara msimu ujao.

Singida United ambao wamepanda daraja msimu huu tangu waliposhuka daraja mwaka 2002 nao watajipima na mabingwa mara tatu mfululizo wa Vpl kwenye tarehe hiyo ambayo tayari imethibitishwa

No comments:

Post a Comment