KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, March 26, 2015

YANGA MWENDO MDUNDO


TIMU ya soka ya Yanga jana iliendelea kudhihirisha makali yake katika michuano ya ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya kuitandika JKT Ruvu mabao 3-1.

Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Yanga ilihesabu bao lake la kwanza dakika ya 33 kupitia kwa mshambuliaji Simon Msuva, aliyeunganisha wavuni kwa shuti kali krosi kutoka pembeni ya uwanja.

Zikiwa zimesalia dakika tatu kuwadia muda wa mapumziko, Yanga ilihesabu bao la pili lililofungwa na Danny Mrwanda, aliyeunganisha pasi kutoka kwa Msuva.

JKT Ruvu ilipata bao la kujifariji dakika ya 45 kupitia kwa Samwel Kamuntu baada ya kupokea pasi akiwa ndani ya mita 18. Mabao hayo yalidumu hadi mapumziko.

Yanga ilihitimisha karamu ya magoli dakika ya 56 baada ya Msuva kufunga bao la tatu kutokana na krosi maridhawa kutoka kwa Mrisho Ngasa.

No comments:

Post a Comment