KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, March 22, 2015

YANGA HAKUNA KULALA


 YANGA imeendelea kujikita kileleni mwa ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya jana kuichapa Mgambo Shooting mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga.

Timu hizo mbili zilicheza kwa kasi katika dakika zote 45 za kipindi cha kwanza, lakini hadi kilipomalizika, hakuna iliyoweza kupata bao.

Baada ya kosakosa kadhaa, Yanga ilihesabu bao lake la kwanza dakika ya 78 kupitia kwa Simon
Msuva baada ya kutokea piga nikupige kwenye lango la Mgambo Shooting.

Dakika tano baadaye, Amis Tambwe aliiongezea Yanga bao la pili baada ya kuunganisha wavuni
kwa kichwa mpira wa krosi uliopigwa na Msuva kutoka pembeni ya uwanja.

Kwa ushindi huo, Yanga inaongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 37 baada ya kucheza mechi
18, ikishinda 11 na kupoteza tatu.

Ligi hiyo inaendelea tena leo wakati Simba itakapomenyana na Ruvu Shooting kwenye Uwanja
wa Taifa, Dar es Salaam wakati Azam itavaana na Coastal Union kwenye uwanja wa Mkwakwani,
Tanga.

No comments:

Post a Comment