KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, August 29, 2012

SERENGETI BOYS SASA KUIVAA MISRI

TIMU ya soka ya taifa ya vijana wa chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) sasa itaivaa Misri katika raundi ya pili ya michuano ya kuwania ubingwa wa Afrika.
Awali, Serengeti Boys ilipangwa kumenyana na Kenya katika raundi ya kwanza ya michuano hiyo iliyotarajiwa kuchezwa Septemba 9 mwaka huu kabla ya nchi hiyo kutangaza kujitoa.
Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, Shirikisho la Soka la Afrika (CAF), limetuma taarifa ya kujitoa kwa Kenya.
Kwa mujibu wa Wambura, pambano la awali kati ya Serengeti Boys na Misri litachezwa Oktoba 14 mwaka huu mjini Dar es Salaam na la marudiano kati ya Oktoba 26-28 mwaka huu nchini Misri.
Mshindi wa mechi hizo mbili atafuzu kucheza raundi ya tatu, ambayo itakuwa ya mwisho kabla ya kwenda Morocco katika fainali zitakazochezwa mwakani.
Katika raundi ya tatu, ambayo mechi zake zitachezwa katikati ya Novemba na za marudiano mwishoni mwa mwezi huo, mshindi kati ya Tanzania na Misri atacheza na mshindi wa mechi kati ya Congo Brazzaville na Msumbiji.

Wachezaji wanaounda kikosi cha Serengeti Boys chini ya Kocha Jakob Michelsen ni makipa Abdallah Bakar (Mjini Magharibi), Hamad Juma (Azam) na Peter Manyika (JKT Ruvu).

Mabeki ni Abdallah Salum (Mjini Magharibi), Basil Seif (Morogoro), Hassan Mganga (Morogoro), Ismail Gambo (Azam), Mgaya Abdul (Azam), Miraji Selemani (Polisi Morogoro), Miza Abdallah (Kinondoni), Mohamed Hussein (Azam), Pascal Matagi (Dodoma) na Paul James (Kinondoni).

Viungo ni Farid Musa (Kilimanjaro), Hussein Twaha (Coastal Union), James Mganda (Kipingu Academy), Mbwana Ilyasa (Simba), Mohamed Haroub (Zanzibar), Mohamed Kapeta (Kinondoni), Mudathiri Yahya (Azam), Mzamiru Said (Morogoro) na Selemani Bofu (JKT Ruvu).

Washambuliaji ni Abdallah Kisimba (Mwanza), Calvin Manyika (Rukwa), Dickson Ambunda (Mwanza), Joseph Lubasha (Azam), Kelvin Friday (Azam) na Salvatory Nkulula (Kipindu Academy).

No comments:

Post a Comment