KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, August 29, 2012

SHARO MILIONEA AMPA SHAVU ALI KIBA

MSANII nyota wa vichekesho na muziki wa kizazi kipya nchini, Hussein Mkieti ‘Sharo Milionea’ amerekodi wimbo mpya kwa kushirikiana na Ali Kiba.
Sharo alisema mjini Dar es Salaam wiki hii kuwa, bado hajaamua kuupa jina wimbo huo.
Alisema awali, walikuwa wameupa jina wimbo huo, lakini baada ya kugundua kwamba limeshatumiwa na wasanii wengine kwenye nyimbo zao, waliamua kulifuta.
“Kwa sasa nasubiri kikao na viongozi wangu ili wanisaidie kupendekeza jina la wimbo huo,”alisema msanii huyo.
Kwa mujibu wa Sharo, iwapo atapendekeza jina la wimbo huo peke yake, huenda lisiwe na mvuto kwa mashabiki na kusababisha apoteze mwelekeo.
Msanii huyo alisema ameamua kumshirikisha Kiba katika wimbo huo kutokana na ukali wake katika fani ya muziki na pia kukubalika na mashabiki.
Alisema kiba ni mmoja wa wasanii nyota nchini katika muziki wa kizazi kipya, hivyo anaamini kwa kushirikiana naye kuimba wimbo huo, utakuwa na mvuto zaidi kwa mashabiki.
Kwa sasa, Sharo anatamba na kibao chake cha ‘Chuki ni Bure’ ambacho amemshirikisha nyota mwingine wa muziki huo nchini, Dully Sykes.
Sharo amewaomba mashabiki wake waendelee kumuunga mkono katika kazi zake ili naye aweze kupata morari ya kufanya vizuri zaidi kwenye gemu.

No comments:

Post a Comment