KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, August 30, 2012

LULU KUBURUTWA TENA KORTI YA RUFANI SEPT 17

NA FURAHA OMARY
MAHAKAMA ya Rufani Tanzania, imepanga kusikiliza shauri la umri wa msanii wa filamu Elizabeth Michael, maarufu kama Lulu, Septemba 17 mwaka huu.
Rufani hiyo iliyokatwa na upande wa Jamhuri kupinga uamuzi wa Jaji Dk. Fauz Twaib kukubali kusikiliza maombi ya kufanyia uchunguzi umri wa Lulu, itasikilizwa na jopo la Majaji watatu.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana katika Mahakama ya Rufani, Majaji waliopangwa kusikiliza shauri hilo ni Jaji Bernard Luanda, Jaji January Msoffe na Jaji Katherine Oriyo.
Lulu anakabiliwa na kesi ya mauaji ya msanii mwenzake Steven Kanumba katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Msanii huyo anadaiwa kutenda kosa hilo, Aprili 7, mwaka huu, nyumbani Kanumba Sinza.
Umri wa msanii huyo umezua utata baada ya mawakili wanaomtetea kudai ana miaka 17 na si 18 kama ilivyodaiwa katika hati ya mashitaka na hivyo kuiomba kesi hiyo isikilizwe katika Mahakama ya Watoto.

Hata hivyo, Mahakama ya Kisutu iliyakataa maombi hayo kwa madai haina uwezo wa kusikiliza shauri hiyo na ndipo mawakili wa Lulu wakawasilisha maombi hayo Mahakama Kuu ambayo katika uamuzi wake ilikubali kufanya uchunguzi wa umri halali wa mshitakiwa huyo.

Hata hivyo siku ambayo Mahakama Kuu ilitarajia kuanza kusikiliza maombi hayo, upande wa Jamhuri uliitarifu kuwa umewasilisha Mahakama ya Rufani maombi ya marejeo ya uamuzi huo.
Kutokana na hilo, Mahakama Kuu aliamua kuahirisha kusikiliza maombi hayo kusubiri uamuzi wa Mahakama ya Rufani.

No comments:

Post a Comment