KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, August 30, 2012

DIAMOND AIBUKA MSHINDI WA NANI MKALI, PROFESA J ASHIKA NAFASI YA PILI

Naseeb Abdul 'Diamond' aibuka mshindi wa nani mkali


Profesa J ashika nafasi ya pili


Ali Kiba ameshika nafasi ya tatu


Ambwene Yesaya AY ameshika nafasi ya tatu kwa kufungana na Kiba


Khamis Mwinjuma 'Mwana FA' ameshika nafasi ya tano


Khaleed Mohamed TID ameshika mkia




MSANII nyota wa muziki wa kizazi kipywa, Naseeb Abdul
'Diamond' ameibuka mshindi wa shindano na msanii yupi mkali wa
kiume wa muziki huo.Diamond ameibuka mshindi wa shindano hilo baada ya
kuwabwaga washiriki wenzake watano.Shindano hilo liliandaliwa na blogu ya liwazo zito na iliendeshwa
kwa muda wa mwezi mmoja kwa wasomaji kuwapigia kura
washiriki.Diamond aliibuka mshindi baada ya kupata kura 21, ambazo ni
sawa na asilimia 45 ya kura zilizopigwa.Mkongwe Joseph Haule, maarufu kwa jina la Profesa J aliibuka
mshindi wa pili baada ya kupara kura nane, sawa na asilimia 17.Nafasi ya tatu ilichukuliwa kwa pamoja na Ali Kiba na Ambwene
Yesaya waliopata kura sita kila mmoja, sawa na asilimia 13. Khamisi Mwinjuma 'Mwana FA' alishika nafasi ya nne baada ya
kupata kura nne, sawa na asilimia nane wakati Khaleed Mohamed
TID alishika mkia baada ya kuambulia kura moja, sawa na asimilia
mbili.Hii ni mara ya sita kwa blogu ya liwazo zito kuendesha shindano la
kuchagua wasanii na wanamichezo bora wa fani mbali mbali ili
kuwawezesha wajitambue mahali walipo na wajue nini la kufanya.Blogu hii inawashukuru wasomaji wake wote walioshiriki kupiga
kura kwa wasanii walioshiriki kwenye shindano hili na kuwaomba
waendeleze ushirikiano huo katika mashindano yajayo.

No comments:

Post a Comment