KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, August 9, 2012

OMOTOLA AMPA TANO MUMEWE

LAGOS, Nigeria
WAKATI filamu yake mpya ya Last Flight to Abuja ikiwa inatamba, mcheza filamu nyota wa kike wa Nigeria, Omotola Jalade amesema anavutiwa na mumewe kutokana na uelewa wake juu ya masuala mbali mbali ya kimaisha.
Omotola alisema wiki hii mjini hapa kuwa, uelewa huo wa mumewe ndiyo ulioiwezesha ndoa yao kudumu kwa miaka 16 hadi sasa na pia kuzaa naye watoto wanne.
Mwanamama huyo mwenye umbo na sura yenye mvuto alisema, licha ya kuvumishiwa skendo mbali mbali, mumewe haonekani kukerwa kwa sababu anafahamu ukweli wa mambo juu yake.
“Nilivutiwa naye tangu tulipokutana kwa mara ya kwanza. Alionekana kunifahamu vyema kuliko nilivyokuwa nikijifahamu. Ni vigumu kuelezea,”alisema.
“Kama nisingefunga ndoa na yeye, nisingeweza kufunga ndoa na mtu mwingine yeyote,”aliongeza mwanadada huyo, ambaye mbali na kucheza filamu, pia ni mwanamuziki.
Omotola alisema amekuwa akizushiwa skendo mbali mbali kutokana na umaarufu wake kwenye fani ya filamu na muziki, lakini kamwe si za kweli.
Alisema yeye ni mtu anayejiheshimu na kamwe hawezi kuvunja utu wake ama kujishusha thamani kwa kufanya vitendo vinavyokiuka maadili ya ndoa.
“Ningekuwa nikijihisi uchungu kama mume wangu angekuwa akiyaweka moyoni mambo hayo na ningekuwa kwenye wakati mgumu. Lakini namshukuru Mungu kwamba huwa hayajali,”alisema Omotola.
Mwanadada huyo alisema alikutana na mumewe kwa mara ya kwanza siku chache baada ya kufiwa na baba yake mzazi na kwamba alipitia kwenye wakati mgumu.
Alisema katika kipindi hicho, alikuwa bado mdogo kiumri, lakini mumewe alikuwa akimpa moyo na kumfanya aweze kuhimili mambo mazito kwa haraka.

No comments:

Post a Comment