KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, August 29, 2012

BANDARI KENYA YAIBANDUA COASTAL UNION

Na Sophia Wakati, Tanga

KIBARUA cha makocha Juma Mgunda na Habibu Kondo leo kimezidi kuwa hatarini baada ya timu yao ya Coastal Union kuchapwa mabao 2-0 na Bandari ya Tanga katika mechi ya kirafiki ya kimataifa iliyochezwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini hapa.

Wachezaji wa Tanzania wanaocheza soka ya kulipwa Bandari ndio walioifungia mabao hayo mawili, la kwanza likiwa limefungwa na David Naftali na la pili na Thomas Maurice.

Mechi hiyo ilikuwa ya pili mfululizo kwa Coastal Union mbele ya mashabiki wake, ambao walionekana kuwa na hasira wakati wa mchezo huo kutokana na timu yao kuonyesha kiwango duni cha soka.

Katika mechi yake nyingine ya kirafiki iliyochezwa mwishoni mwa wiki iliyopita, Coastal Union ilichapwa mabao 2-1 na Polisi Morogoro kabla ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya JKT Oljoro.

Coastal Union inatarajiwa kushuka tena dimbani Jumamosi kumenyana na Yanga kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment