KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, August 29, 2012

GENEVIEVE AVISHWA PETE YA UCHUMBA

LAGOS, Nigeria
MCHEZA filamu nyota wa Nigeria, Genevieve Nnaji amevishwa pete ya uchumba na anatarajia kufunga ndoa hivi karibuni.
Habari za kimtandao zimeeleza kuwa, tayari Genevieve ameshavishwa pete ya uchumba na mumewe mtarajiwa hivi karibuni.
Hata hivyo, Genevieve hayupo tayari kumtaja mchumba wake huyo kwa madai kuwa, anataka kuwashangaza mashabiki wake.
Genevieve amekaririwa kupitia akaunti yake ya twitter wiki hii akisema kuwa, baada ya muda si mrefu anatarajia kuitwa ‘mke wa mtu’.
“Natarajia kuitwa mke hivi karibuni,” alisema msanii huyo kupitia kwenye mtandao huo.
Genevieve, ambaye ni mama wa mtoto mmoja pia aliandika kwenye mtandao huo maneno yasemayo: “busu maalumu kwa ajili yako.”
Mwanadada huyo mwenye sura yenye mvuto pia aliweka picha yake kwenye mtandao huo, ikimuonyesha akiwa amevaa pete ya uchumba.
Msanii huyo amekuwa akitajwa kuwa na uhusiano wa mapenzi na mwanamuziki maarufu wa Nigeria, D’Banj.
Hata hivyo, wote wawili wamekuwa wakikanusha mara kwa mara taarifa hizo na kudai kuwa, uhusiano wao ni wa kawaida, kama ule wa kaka na dada.

No comments:

Post a Comment