KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, August 9, 2012

INI EDO AKIRI KUWA NA UJA UZITO

LAGOS, Nigeria
BAADA ya ukimya wa muda mrefu, hatimaye mcheza filamu tajiri wa kike nchini Nigeria, Ini Edo amethibitisha kuwa ni kweli ana uja uzito.
Ini amethibitisha ukweli huo katika mahojiano yaliyochapishwa hivi karibuni kati yake na gazeti la E 24-7 la Nigeria.
Uamuzi wa Ini kuthibitisha taarifa hizo, umekuja siku chache baada ya baadhi ya vyombo vya habari vya Nigeria kuripoti kuwa, yeye na Mercy Johnson ni waja wazito.
Vyombo hivyo vya habari pia viliripoti kuwa, Ini na Mercy wamepanga kujifungulia nchini Marekani, ambako ndiko waume zao wanakoishi.
Siku chache baada ya kuripotiwa kwa taarifa hizo, Ini alizikanusha kwa madai kuwa hazikuwa za kweli. Ini alifunga ndoa na Philip Ehiagwina mwaka 2008.
Kwa mujibu wa taarifa za mitandao, Ini na Mercy wanatarajiwa kujifungua hivi karibuni.
Ini na Mercy wanatarajiwa kwenda Marekani mara baada ya kukamilisha kazi ya kucheza filamu yao mpya, inayorekodiwa katika mji wa Asaba uliopo kwenye jimbo la Delta.
Mume wa Ini, Philip ni mfanya biashara anayeishi Marekani. Mercy na mumewe, Prince Odi Okoije walifunga ndoa Agosti 2011.

No comments:

Post a Comment