KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, August 15, 2012

Shule 93 za Sekondari kufaidika na mradi wa Vitabu wa Airtel

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano wa Kampuni ya Simu ya Airtel Tanzania,Beatrice Singano Mallya (katikati) akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya dhamira ya kampuni hiyo kusaidia elimu kwa kuzipatia vitabu shule mbali mbal za sekondari,wakati wa kuchezeshwa droo iliyozipata shule 93 hapa nchini.kulia ni Meneja wa Mahusiano ya Jamii wa Airtel,Hawa Bayumi na kushoto ni Afisa Mkuu Mwandamizi wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA),Masozi Nyirenda.

Meneja wa Mahusiano ya Jamii wa Airtel,Hawa Bayumi akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati akisoma majina ya shule zitakazofanikiwa kupitiwa na mradi huo mara baada ya droo iliyochezeshwa leo kwenye makao makuu ya kampuni hiyo ya Airtel,jijini Dar.

Kutoka kushoto: Afisa Mkuu Mwandamizi wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA),Masozi Nyirenda,Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano wa Kampuni ya Simu ya Airtel Tanzania,Beatrice Singano Mallya na Meneja wa Mahusiano ya Jamii wa Airtel,Hawa Bayumi wakionyesha baadhi ya vitabu vitakavyokabidhiwa kwa shule 93 zilizofanikiwa kushinda katika droo hiyo iliyochezeshwa leo kwenye makao makuu ya Kampuni ya Airtel Tanzania,jijini Dar es Salaam leo.


Afisa Mkuu Mwandamizi wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), Masozi Nyirenda akitoa shukrani kwa Kampuni ya Airtel kwa kusaidia kukuza elimu hapa nchini.

Airtel Tanzania, leo imeendeleza dhamira yake katika kuboresha elimu kwa kuchezesha droo iliyochagua shule za sekondari 93 zitakazo faidika na mradi wa vitabu wa Airtel wa kusaidia jamii unaojulikana kama Airte shule yetu kwa mwaka 2012 -2013
Akiongea katika mkutano na vyombo vya Habari Mkurugenzi wa Airtel Kitengo cha Mawasiliano Bi, Beatrice Singano Mallya alisema “Mwaka huu , Airtel tunaendelea na dhamira yetu ya kusaidia elimu kwa kuzipatia vitabu shule za sekondari 93, Mradi huu utafaidisha shule 3 kutoka katika kila mkoa Tanzania bara na visiwani.
Shule 93 zilizo chaguliwa leo ni matokeo ya droo iliyochezeshwa na kuzichagua shule hizo kutoka shule 3,000 zilizopendekezwa na Wizara ya Elimu Tanzania kuwa ni shule ambazo zina uhitaji mkubwa wa vitabu na kushauri ziingie katika mpango wa kusaidia jamii wa Airtel shule yetu.
“Toka tulivyooanza mradi huu wa Vitabu miaka saba iliyopita tumeweza kuzifikia zaidi ya shule 1000 za sekondari zilizopo Tanzania bara na visiwani kwa kutoa msaada sawa kwa mikoa yote na kuwafikia wanafunzi katika kila kona ya Tanzania.
Mwaka huu vitabu tunavyogawa vinakadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya shilingi milioni 110, hivyo kila shule iliyopatikana kwenye droo hii watapata Vitabu alisema Mallya
Bi Mallya aliongeza kwa kusema “tumefanya kazi kwa pamoja na Mamlaka ya elimu na Wizara ya Elimu Tanzania kwa kuhakikisha kwamba mahitaji ya vitabu kwa shule zote zitakazoingia kwenye Mradi huu wa Shule yetu tunayatimiza kwa kuwapatia vitabu vya mitaala ya masomo yao kama ilivyopendekezwa na Wizara”
“Airtel Tanzania imekuwa mstari wa mbele kwa kutoa misaada mbalimbali ili kuisaidia jamii hapa Tanzania hasa kwa kuchangia sekta ya elimu kwa kuwapatia vitendea kazi vikiwemo Vitabu kwa wanafunzi wa shule za sekondari.
Mwaka jana pia Airtel ilisaidia Vitabu vyenye thamani ya zaidi ya milioni 104 tsh kwa shule za sekondari kwa kupitia droo iliyohusisha jumla ya shule 502” alisema Bi, Mallya.
Nae Afisa Mkuu Mwandamizi wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) Bw Masozi Nyirenda aliongea kwa Niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Ulimu (TEA) alisema “Mamlaka ya Elimu Tanzania tunawashukuru sana Airtel kwa dhamira yenu ya kusaidia jamii kwa kuinua kiwango cha elimu hapa nchini ” Mradi wa Airtel Shule Yetu ni mradi mzuri sana kwa jamii yetu kwa kuinua kiwango cha elimu na maisha ya watanzania”
Tunaamini elimu ndio ufunguo wa maisha hivyo watanzania wote pamoja na waalimu mtakaopokea vitabu hivi vya mradi wa Airtel Shule yetu tuvitunze na kuvitumia vizuri ili kuunga mkono jitihada za Airtel katika kusaidia kuinua kiwango cha elimu hapa nchini” aliongeza kwa kusema Bw, Nyirenda
Mbali na shule 93 za sekondari zitakazofaidika na mradi huu wa vitabu mwaka huu, pia Airtel Tanzania imeshamaliza kukarabati shule ya msingi ya Kiromo iliyopo nje kidogo ya jiji la DSM kando kando na barabara ya bagamoyo ilichaguliwa mwaka jana 2011 huku mipango mingine ya mwaka huu ikiendelea ili kupata shule nyingine itakayofaidika kwa kujengwa na kukarabatiwa na Airtel shule Yetu
Airtel bado itaendelea kushirikiana wizara ya elimu kwa wadau wengine kuweza kushiriki katika kuinua kiwango cha elimu hapa Tanzania.

No comments:

Post a Comment