KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, August 30, 2012

DIWANI ILALA ATEMBELEA KAMBI ZA MISS UTALII ZA KINONDONI NA ILALA



DIWANI wa kata ya mchikichini na Mwenyekiti wa Madiwani wa
kata tano (Ilala, Mchikichini, Kariakoo, Gerezani na Jangwani),
Ghalib Riyami ametembelea kambi ya washiriki wa
Miss Utalii wilaya ya Ilala na Kinondoni 2012.

Kambi hiyo ya pamoja kati ya warembo wanao
wania taji la Miss Utalii Ilala 2012 na wale wanao wania taji la Miss
Utalii Kinondoni 2012 ipo katika hoteli ya kitalii ya nyota tatu ya
Lamada Hotel.
Diwani huyo ameelezea kufurahishwa kwake kwa wilaya ya
Ilala kupewa heshima ya kuwa wenyeji wa shindano hilo la
kihistoria ambapo wilaya mbili kwa pamoja zinashindana kuwania
mataji ya wilaya zao katika ukumbi na steji moja tena siku moja.
“Najua waandaaji wangeweza kuamua shindano hili lifanyikie
kinondoni,lakini mmeamua kutupa heshima hiyo sisi wa wilaya ya
ilala,hakika tumefarijika sana,” alisema.

Katika kuonyesha furaha yake na kupokea heshima hiyo aliyoiita

kubwa, diwani huyo aliahidi kuwa yeye binafsi pamoja na

madiwani wa wilaya ya ilala watahakikisha wanasaidia na kuunga

mkono kwa hali na mali kufanikisha kufanyika kwa shindano hilo

kama lilivyopangwa yaani tarehe 14/09/2012 katika hotel ya Lamada.
Aliwataka warembo wanaoshiriki shindano hilo kutambua kuwa
shindano hili tofauti na mashindano mengine ni alama ya urithi wa
Taifa na kielelezo cha utamaduni wa mtanzania,hivyo wanapaswa
kutambua kuwa na nidhamu na kuvaa uhalisia wa mtanzania siku
zote na wakati wote mashindanoni nan je ya mashindano.
Amewakumbusha na kuwaomba kutumia shindano hili kutangaza
utalii wa wilaya ya Ilala na mkoa kwa ujumla ikiwemo uwanja wa

ndege wa Juliasi Nyerere, soko la Kariakoo, Makumbusho ya
Taifa, soko la kimataifa la samaki la Magogoni, shule ya Pugu
ambayo Mwalimu Nyerere alifundisha, na ufukwe wa bahari ya
hindi.
Diwani huyo aliwashukuru na kuwapongeza wadhamini
mbali mbali ambao wamethibitisha kudhamini shindano
hili,wakiwemo Lamada Hotel,105 Times FM Radio,Kahama Gold
Mine,Traventine Hotel,Mzee Yusuph Enterprises,Easy Media,Daja
Saloon,Zizu Fashion,Tambaza Cort Brocker and Action Mart,Dagaa
Finance na Aucland Travel and Tours,Hameed Designer.

Ametoa wito kwa kampuni na watu mbali mbali
kudhamini na kuchangia shindano hili ambalo gharama za kuandaa
ni kubwa hivyo kuhitaji mchango wa hali na mali.
Jumla ya warembo ishirini na nne(24), kumi na mbili kutoka wilaya ya
Kinondoni na kumi na mbili kutoka wilaya ya Ilala kwa pamoja
watachuana ili kupata taji la Miss Utalii wa wilaya ya Ilala na Miss
Utalii wilaya ya Kinondoni.

Wilaya ya Ilala washiriki ni Zourha Malisa, Nancy Musheruzi,

Princess Lemi, caroline Yust, Eunice George, Naomi Michael, Lucy Julius,

Nurina Mikindo, Rose James, Salome Kiula, Marry Wambura na Judith Frank.

Washiriki wa wilaya ya Kinondoni ni Mwasiti Thabit, Irene Richard,

Hellen Herman, Fatma Hussein, Rachel Magai, Neema Mbeju,
Neema Ngowi, Duda Tumbo, Zahra Waziri, Janeth Nelson,

Teddy Paul na Ruby Kivunjo.
Akizungumza na warembo hao muheshimiwa diwani alisisita
umuhimu wa warembo hawa kulitumikia taifa kwa kutangaza
vivutio vya kitalii kitaifa na kimataifa ili kusaidia kuinua uchumi na
kuongezeka kwa pato la taifa wakati huu ambapo sekta ya utalii
inachangia asilimia zaidi ya kumi na saba(17%) ya pato la taifa.
Alisisitiza umuhimu wa kuelimisha vijana mashuleni ili kukuza na
kuhamasisha utalii wa ndani pia alisisitiza haja ya kutangaza kwa
nguvu zote vivutio vya utalii vya nchi yetu ya Tanzania ili kuongeza
idadai ya watalii wanaotembelea, ikiwa hadi leo kulingana na
takwimu Tanzania hutembelewa na watalii laki nane(800,000) kwa
mwaka na hii ni idadi ndogo ukilinganisha na nchi jirani
zinazotuzunguka.
Pia alitoa wito kwa wazazi kuondokana na dhana potofu juu ya
mashindano ya urembo na aliwaasa mabinti kuwa na heshima,
adabu na haiba nzuri ili kuifanya jamii kubadili mtazamo juu ya
mashindano haya yenye tija kwa taifa letu kwa kuwa linatangaza
utalii wa taifa hili la Tanzania.
Mwisho aliahidi ushirikiano wa hali na mali katika kufanikisha
shindano hili ambalo limepangwa kufanyika katika ukumbi wa
lamada hotel ambao upo katika umoja wa kata tano
anazoziongoza.

No comments:

Post a Comment