KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, August 13, 2012

AFC LEOPARDS YA KENYA KUKIPIGA NA SIMBA, YANGA IDD EL FITR

TIMU ya soka ya AFC Leopards ya Kenya inatarajiwa kuja nchini wiki hii kucheza mechi mbili za kirafiki za kimataifa dhidi ya Simba na Yanga.

Mechi hizo mbili zimeandaliwa na Kampuni ya Dar Solutions kwa ajili ya kuzipa mazoezi Simba na Yanga zinazojiandaa kwa michuano ya ligi kuu ya Tanzania Bara.

Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Kenny Mwaisabula alisema mjini Dar es Salaam leo kuwa, AFC Leopards itacheza mechi yake ya kwanza Agosti 19 kwa kupambana na Simba kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha.

Kwa mujibu wa Mwaisabula, AFC Leopards itajitupa tena uwanjani Iddi Pili (Agosti 21) kwa kumenyana na Yanga kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Wakati huo huo, Mwaisabula alisema timu ya Coastal Union inatarajiwa kupimana ubavu na Chemili ya Kenya katika mechi ya kirafiki ya kimataifa itakayochezwa siku ya Iddi Mosi kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga.

No comments:

Post a Comment