KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, August 31, 2012

MBUYU TWITE KUTAMBULISHWA LEO U/TAIFA DAR

Beki mpya wa Yanga, Mbuyu Twite akipewa maelekezo na Kocha Tom Saintfiet wakati wa mazoezi yaliyofanyika jana kwenye uwanja wa shule ya sekondari ya Loyola mjini Dar es Salaam.

Mbuyu Twite akiwa katika mazoezi ya Yanga yaliyofanyika jana kwenye uwanja wa shule ya sekondari ya Loyola.


BEKI mpya wa klabu ya Yanga, Mbuyu Twite anatarajiwa kutambulishwa rasmi leo kwa mashabiki wa klabu hiyo.

Kocha Tom Saintfiet wa Yanga amepanga kumtambulisha beki huyu wakati wa mechi ya kirafiki ya soka dhidi ya Coastal Union itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Twite aliwasili nchini juzi akitokea Rwanda na kumaliza wasiwasi uliokuwa umetanda kwamba huenda angeshindwa kujiunga na timu hiyo baada ya kudaiwa kuwa aliitapeli Simba.

Hata hivyo, hakuna uhakika iwapo Twite atacheza mechi hiyo kutokana na kutofanya mazoezi na wenzake kwa muda mrefu.

No comments:

Post a Comment