KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, August 29, 2012

MTANZANIA AOMBEWA ITC UJERUMANI

CHAMA cha Soka cha Ujerumani (DFB) kimetuma maombi ya kupatiwa hati ya uhamisho wa kimataifa (ITC) kwa ajili ya mchezaji Robert Makanja. DFB imetuma maombi hayo kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ili kumwezesha mchezaji huyo kuichezea timu ya TUS Ahausen, Hessischer FuBall-Verband ya Ujerumani.
Hata hivyo, DFB haikueleza timu hiyo inashiriki ligi ya daraja gani nchini humo. Wambura alimkariri Mkuu wa Mashindano wa DFB, Markus Stenger akisema kuwa, Mtanzania huyo ameombewa hati hiyo kama mchezaji wa ridhaa kwa maelezo kuwa hakuwahi kusajiliwa na klabu yoyote nchini.

Alisema TFF inayafanyia kazi maombi hayo na hati hiyo itatolewa mara baada ya taratibu husika kukamilika, ikiwemo kubaini kama kweli mchezaji huyo hakuwahi kusajiliwa na klabu yoyote hapa nchini.

No comments:

Post a Comment