KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, August 29, 2012

NGASA, AKUFFOR WAIBEBA SIMBA

Na Shaaban Mdoe, Arusha
MABINGWA wa soka nchini Simba leo wameendelea kudhihirisha jinsi kikosi chao kilivyo moto baada ya kuichapa JKT Oljoro mabao 2-1 katika mechi ya kirafiki iliyochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Arusha.

Ushindi huo ulikuwa wa pili mfululizo kwa Simba katika kipindi cha siku nne. Mwishoni mwa wiki iliyopita, Simba iliilaza Mathare United mabao 2-1 katika mechi ya kirafiki ya kimataifa iliyochezwa kwenye uwanja huo.
Mshambuliaji Mrisho Ngasa alikuwa miongoni mwa wachezaji walioifungia Simba mabao hayo mawili, likiwa bao lake la kwanza tangu aliposajiliwa na mabingwa hao msimu huu akitokea Azam FC.

Bao la pili la Simba lilifungwa na mshambuliaji mpya kutoka Ghana, Daniel Akuffor, likiwa bao lake la pili tangu alipoanza kuichezea timu hiyo.

Akuffor aliifungia Simba bao la kwanza dakika ya 25 baada ya kuunganisha wavuni pasi ya Ngasa kabla ya Ngasa kuongeza la pili dakika ya 76 baada ya kupokea pasi kutoka kwa Abdalla Juma.

Oljoro JKT ilipata bao la kujifariji dakika ya 89 lililofungwa kwa njia ya penalti na Markus Mpangala baada ya beki Paschal Ochieng wa Simba kumuangusha mchezaji huyo ndani ya eneo la hatari.

No comments:

Post a Comment