KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, September 30, 2012

NIZAR KHALFAN AIBEBA YANGA, YAICHARAZA AFRICAN LYON 3-1


YANGA leo imeendelea kuchanja mbuga katika michuano ya soka ya ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya kuicharaza African Lyon mabao 3-1 katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mshambuliaji Nizar Khalfan ndiye aliyeibeba Yanga baada ya kuifungia mabao mawili katika kipindi cha pili. Nizar aliingia kipindi hicho kuchukua nafasi ya Frank Domayo.
Yanga ilikuwa ya kwanza kupata bao katika kipindi cha kwanza lililofungwa na mshambuliaji Didier Kavumbagu. Bao hilo lilidumu hadi mapumziko.
Benedicto Mwalangali aliisawazishia African Lyon dakika za mwanzo za kipindi cha pili kabla ya Nizar kufunga la pili na kuongeza la tatu.

Matokeo hayo yameiwezesha Yanga kushika nafasi ya nne katika msimamo wa ligi hiyo, ikiwa na pointi saba baada ya kucheza mechi nne.
Simba inaongoza ligi hiyo kwa kuwa na pointi 12 baada ya kucheza mechi nne, ikifuatiwa na Azam yenye pointi 10 na Coastan Union yenye pointi saba, sawa na Yanga.

No comments:

Post a Comment