KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, September 22, 2012

YANGA YATANGAZA RASMI KUMTIMUA SAINTFIET


HATIMAYE klabu ya Yanga imetangaza rasmi kumtimua kocha mkuu wa timu hiyo, Tom Saintfiet kutoka Ubelgiji.
Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Clament Sanga ametangaza maamuzi hayo leo asubuhi alipozungumza na waandishi wa habari makao makuu ya klabu hiyo mitaa ya Twiga na Jangwani, Dar es Salaam.
Sanga alisema nafasi ya Saintfiet itashikiliwa kwa muda na kocha msaidizi, Fred Felix Minziro hadi atakapotafutwa kocha mwingine.
Kwa mujibu wa Sanga, kocha huyo ametimuliwa kutokana na matokeo mabaya ya Yanga katika mechi za ligi kuu ilizocheza hivi karibuni, ambapo ililazimishwa kutoka suluhu na Prisons kabla ya kunyukwa mabao 3-0 na Mtibwa Sugar.

Sanga alisema si kweli kwamba wamemtimua Saintfiet kutokana na kutokuelewana na mwenyekiti wa klabu hiyo, Yussuf Manji.
Makamu mwenyekiti huyo wa Yanga alizitaja sababu zingine zilizochangia kutimuliwa kwa kocha huyo kuwa ni pamoja na kujihusisha na vitendo vya ulevi akiwa na wachezaji wa timu hiyo.
"Yapo mapungufu mengine mengi, lakini hatuwezi kuyaweka hadharani,"alisema.
Sanga alisema pia kuwa, nafasi ya katibu mkuu wa klabu hiyo kwa sasa itashikwa kwa muda na Lawrence Mwalusako wakati Dennis Oundo ameteulia kuwa mkurugenzi wa fedha na utawala.
Mwalusako amechukua nafasi ya Celestine Mwesigwa, ambaye mkataba wake umesitishwa sambamba na aliyekuwa ofisa habari, Louis Sendeu.
Yanga pia imeteua Sekilojo Chambua kuwa meneja mpya wa timu hiyo, kuchukua nafasi ya Hafidh Saleh, ambaye  atapangiwa majukumu mengine.

No comments:

Post a Comment