KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, September 21, 2012

SILAHA ZA YANGA KWA JKT RUVU, JE MINZIRO ATABADILI KIKOSI BAADA YA TOM KUTIMULIWA?


KOCHA Mkuu wa Yanga. Tom Saintefiet ametangaza kikosi cha wachezaji 18 watakaocheza mechi ya ligi kuu ya Tanzania bara kesho dhidi ya JKT Ruvu itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Katika kikosi hicho, Tom ameamua kumtema mshambuliaji nyota wa timu hiyo, Saidi Bahanunzi na kumpa nafasi hiyo, Jerry Tegete.
Tom aliwaambia waandishi wa habari mjini Dar es Salaam jana kuwa, amekuwa akikatishwa tamaa na tamaa na baadhi ya wachezaji wake kutokana na viwango vyao kushuka.
Kocha huyo kutoka Ubelgiji alisema katika mazoezi waliyofanya leo asubuhi ya upigaji wa penalti, kati ya wachezaji sita waliopiga adhabu hiyo, waliofunga ni wawili tu.
Aliwataja wachezaji aliowateua kwa ajili ya mechi ya kesho, ambayo itakuwa ya tatu tangu kuanza kwa
ligi kuu kuwa ni makipa; Yaw Berko, Ally Mustafa ‘Barthez’, mabeki Juma Abdul, Godfrey Taita, Mbuyu Twite, Kevin Yondan, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Ladislaus Mbogo, Oscar Joshua na Stefano Mwasika.
Viungo ni Athumani Iddi ‘Chuji’, Haruna Niyonzima, Nizar Khalfan, Rashid Gumbo, Shamte
Ally na Simon Msuva wakati washambuliaji ni Jerry Tegete, Didier Kavumbangu na Hamisi Kiiza.
Wachezaji walioachwa kwenye kikosi hicho ni kipa Said Mohamed, mabeki Nsajigwa Shadrack, Job
Ibrahim, viungo Frank Domayo, Juma Seif ‘Kijiko’, Salum Telela, Omega Seme, Nurdin Bakari, Idrisa
Assega na Issa Ngao.

No comments:

Post a Comment