KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, September 11, 2012

SIMBA YATWAA NGAO YA JAMII, YAIBANJUA AZAM 3-2

Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Makongoro Mahanga (kulia) akimkabidhi ngao ya jamii, nahodha wa Simba, Juma Kaseja baada ya timu hiyo kuichapa Azam mabao 3-2 katika mechi iliyopigwa leo jioni kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

SIMBA leo imefanikiwa kutwaa Ngao ya Jamii baada ya kuicharaza Azam FC mabao 3-2 katika mechi iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mechi hiyo ni maalumu kwa ajili ya ufunguzi wa michuano ya ligi kuu ya Tanzania Bara, inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Jumamosi.
Ushindi huo ulikuwa wa kulipiza kisasi kwa Simba kufuatia kuchapwa mabao 3-1 na Azam katika mechi ya nusu fainali ya Kombe la Kagame.
Azam ilikuwa ya kwanza kupata mabao kupitia kwa John Bocco na Kipre Tchetche kabla ya Daniel Akuffour kuifungia Simba bao dakika chache kabla ya mapumziko na kuyafanya matokeo yawe 2-1.
Simba ilibadili mchezo kipindi cha pili na kufanikiwa kusawazisha kwa bao lililofungwa na Emmanuel Okwi kabla ya Mwinyi Kazimoto kuongeza la tatu na la ushindi.

No comments:

Post a Comment