KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, September 26, 2012

WAREMBO MISS TANZANIA KAMBINI OKT 2


WAREMBO 30 watakaoshiriki katika shindano la mwaka huu la kuwania taji la Miss Tanzania, wanatarajiwa kuingia kambini Oktoba 2 mwaka huu kwenye hoteli ya Giraffe mjini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania, Hashim Lundenga alisema jana kuwa, shindano la mwaka huu limepangwa kufanyika Novemba 3 mwaka huu kwenye hoteli ya Blue Pearl mjini Dar es Salaam.
Lundenga alisema washiriki wa shindano hilo wamepatikana baada ya kukamilika kwa mashindano ya awali ya ngazi ya mkoa na kanda.
Mwenyekiti huyo wa Miss Tanzania alisema mashindano ya mwaka huu yalikuwa na msisimko mkubwa kutokana na kuwashirikisha wasichama wengi wasomi wa elimu ya juu.
"Tunaamini mashindano ya mwaka huu ya Miss Tanzania yatakuwa na ushindani mkali kutokana na asilimia 90 ya washiriki kuwa wasomi wa vyuo vya elimu ya juu,"alisema.
Meneja wa kinywaji cha Redd's, ambao ni wadhamini wakuu wa shindano hilo, Victoria Kimaro alisema wamejipanga vyema kuhakikisha shindano la mwaka huu linakuwa na mvuto wa aina yake.
Alisema lengo la wadhamini ni kuona kuwa, mashabiki wa fani hiyo wanapata burudani ya aina yake na mshindi mwenye sifa na vigezo vya kuiwakilisha vyema Tanzania katika shindano la dunia.
Victoria alisema wakati watakapokuwa kambini, washiriki watajifunza mambo mbali mbali kwa kuzingatia mabadiliko ya kalenda ya mashindano ya urembo ya dunia.
Kutokana na mabadiliko hayo, alisema mrembo wa Tanzania atakuwa na muda mrefu wa maandalizi na atatakiwa kuripoti katika fainali za mashindano ya urembo ya dunia mwakani.

No comments:

Post a Comment