KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, September 26, 2012

OMOTOLA: SIJAKUZA MAKALIO YANGU


LAGOS, Nigeria
MWANAMUZIKI na mcheza filamu mwenye mvuto nchini Nigeria, Omotola Jalade amekanusha madai kuwa, amefanyiwa operesheni maalumu kwa ajili ya kukuza makalio yake.
Omotola amekaririwa na mtandao mmoja wa Nigeria wiki hii akisema kuwa, taarifa hizo ni za uzushi na hazina ukweli wowote.
Baadhi ya mitandao ya Nigeria iliripoti hivi karibuni kuwa, Omotola amekuza makalio yake baada ya kuchapishwa kwa picha zake akiwa mjini Lagos hivi karibuni akionekana amejazia.
Mitandao hiyo ilidai kuwa, mwanamama huyo ameamua kufanya operesheni hiyo kwa lengo la kuongeza mvuto wa mwili wake.
Hata hivyo, Omotola ameziita taarifa hizo kuwa ni za uzushi kwa vile kuongezeka kwa makalio yake ni matokeo ya kunenepa kwa mwili wake.
"Kamwe siwezi kufanya kitu kama hicho. Hili ni umbile langu halisi. Ndivyo mwili wangu ulivyo. Ninaonekana tofauti kwa sababu nimeongezeka uzito,"alisema.
Amewataka mashabiki wake waache kuziamini taarifa hizo kwa sababu anafurahia uumbaji wa Mungu kwake na hawezi kufanya kitu kingine tofauti kwa lengo la kuongeza mvuto.

No comments:

Post a Comment