KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, September 23, 2012

SIMBA YAZIDI KUCHANUA, YAICHAPA RUVU SHOOTING 2-1


BAO lililofungwa na mshambuliaji chipukizi, Christopher Edward leo limeiwezesha Simba kuichapa Ruvu Shooting mabao 2-1 katika mechi ya ligi kuu ya Tanzania Bara iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam
Edward aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Ramadhani Chombo, alifunga bao hilo dakika 10 kabla ya mchezo kumalizika, kufuatia kazi nzuri iliyofanywa na Mrisho Ngasa.
Simba ilikuwa ya kwanza kupata bao kupitia kwa Felix Sunzi, aliyeunganisha wavuni kwa kichwa krosi maridhawa iliyochongwa na Nassoro Masoud Chollo aliyepanda mbele kusaidia mashambulizi.
Ruvu Shooting ilisawazisha bao hilo dakika ya 78 kwa bao lililofungwa na Seif Rashid baada ya kumpokonya mpira beki Juma Nyoso ndani ya eneo la hatari na kuukwamisha mpira wavuni.
Simba ilifanikiwa kupata penalti kipindi cha kwanza baada ya beki mmoja wa Ruvu Shooting kuunawa mpira ndani ya eneo la hatari, lakini shuti la Daniel Akuffour lilipanguliwa na kipa Benjamin Haule na kuwa kona, ambayo haikuzaa matunda.

No comments:

Post a Comment