KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, September 26, 2012

DESMOND ELLIOT AZUSHIWA KIFO



LAGOS, Nigeria
MCHEZA filamu machachari wa Nigeria, Desmond Elliot amejikuta akiwa kwenye wakati mgumu baada ya kuzushiwa mara kwa mara kwamba ameuawa.
Uvumi wa kifo cha Elliot umekuwa ukienezwa kupitia kwenye mitandao mbali mbali ya kijamii na baadhi ya mashabiki wameonekana kukerwa na uzushi huo.
Septemba 14 mwaka huu, mtu mmoja aliandika kupitia kwenye facebook kwamba Elliot ameuawa na kuweka picha inayofanana na ya Elliot.
Lakini mwisho wa maelezo hayo, mtu huyo aliandika: "Tafadhali msishtke kwa sababu picha hii ni sehemu ya filamu mpya (ya Elliot), ambayo bado haijatoka."
Elliot ameungana na watu wengine maarufu nchini Nigeria, Morgan Freeman na Bill Nye ambao mapema mwezi huu nao walizushiwa vifo, lakini ikaja kubainika baadaye kwamba taarifa hizo hazikuwa za kweli.
Mapema wiki hii, mtu mwingine aliweka kwenye mtandao wa facebook picha ya mtu akiwa amelala kwenye dimbwi la damu na kuandika: "Habari zilizotufikia hivi punde: Mwigizaji wa Nigeria,Desmond Elliot amekutwa akiwa hajiwezi kwenye dimbwi la damu kwenye hoteli moja mjini Lagos."
Taarifa hiyo feki iliendelea kudai kuwa, Elliot alikuwa ameuawa kwenye chumba cha hoteli hiyo na kwamba uchunguzi juu ya mtu aliyemuua ulikuwa ukiendelea kufanywa na polisi.
Mwisho wa taarifa hiyo, mtu huyo aliandika: "Tafadhali msishtuke kwa sababu hii ni sehemu ya filamu mpya, ambayo bado haijatoka."
Mitandao mingine iliendelea kusambaza taarifa hizo feki na kuwapa usumbufu mkubwa mashabiki wa filamu, wakiwa wameondoa maneno ya mwisho yanayosema: "Tafadhali msishtuke."

No comments:

Post a Comment