KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, September 21, 2012

SANGA AKIRI KUTIMULIWA KWA MAOFISA YANGA


UONGOZI wa klabu ya Yanga umeisimamisha kazi sekretarieti nzima ya klabu hiyo,

akiwemo Katibu Mkuu, Celestine Mwesigwa na Ofisa Habari, Louis Sendeu kutokana na kilichodaiwa kuwa ni utendaji mbovu wa kazi.
Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga aliwaambia waandishi wa habari mjini Dar es Salaam leo kuwa, uamuzi huo umefikiwa katika kikao cha kamati ya utendaji ya klabu hiyo kilichofanyika kuanzia asubuhi hadi jioni.
Watendaji wengine wa Yanga waliokutwa na pangua pangua hiyo ni aliyekuwa ofisa wa utawala, 
Masoud Saad, aliyekuwa mhasibu, Philip Chifuka na aliyekuwa meneja wa muda wa timu, Hafidh Saleh.
“Ni kweli tumeamua kusitisha mikataba ya sekretarieti nzima, pia tumefanya marekebisho, tumewatoa baadhi ya watendaji na kuteua watendaji wapya,”alisema Sanga.

No comments:

Post a Comment