KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, September 21, 2012

BREAKING NEWSSSSS! KOCHA MKUU YANGA, KATIBU MKUU WATIMULIWA


UONGOZI wa klabu ya Yanga umetangaza kuwatimua Kocha Mkuu wa timu hiyo, Tom Saintfiet, Katibu Mkuu, Celestine Mwesigwa na Ofisa Habari, Louis Sendeu.
Uamuzi huo ulifikiwa katika kikao cha kamati ya utendaji ya klabu hiyo kilichofanyika mjini Dar es Salaam leo.
Kikao hicho kiliitishwa siku moja baada ya Yanga kuchapwa mabao 3-0 na Mtibwa Sugar katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Kipigo hicho kilikuwa mwendelezo mbaya kwa Yanga katika ligi hiyo iliyoanza wiki mbili zilizopita. Katika mechi ya ufunguzi, Yanga ililazimishwa kutoka suluhu na Prisons kwenye uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.

No comments:

Post a Comment