KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, September 26, 2012

RITA: SINA MATATIZO NA INI EDO


LAGOS, Nigeria
MCHEZA filamu nyota wa Nollywood, Rita Dominic amesema hana matatizo na msanii mwenzake wa fani hiyo, Ini Edo.
Rita alisema wiki hii kupitia mtandao wa facebook kuwa, tuhuma zinazoenezwa kuwa haelewani na Ini Edo hazina ukweli wowote.
"Sina tatizo lolote na Ini Edo linalohitaji kupatanishwa. Msiamini kila mnachokisoma kwenye vyombo vya habari,"ameeleza Rita kupitia mtandao huo.
Rita ametoa ufafanuzi huo baada ya shabiki wake mmoja kumuuliza kupitia mtandao huo ni lini atamaliza tofauti kati yake na Ini.
Ini na Rita wamekuwa wakiripotiwa kuwa na tofauti tangu mwaka 2011, lakini mara zote wamekuwa wakikanusha madai hayo.
Tuhuma hizo ziliibuka kwa mara ya kwanza baada ya nyota hao wawili kuteuliwa kuwania tuzo za waigizaji bora wa AFRIFF za mwaka 2011.
Rita na Ini walikuwa wakiwania tuzo ya mwigizaji bora wa kike na mshindi alitakiwa kusafiri kwenda London mwaka unaofuata. Tuzo hizo zilidhaminiwa na Arik Airline.
Kabla ya kutolewa kwa tuzo hizo, Rita alilalamikia kitendo cha Ini kuingilia kati mchakato wa uteuzi wa washindi kwa kuandika kwenye mtandao wa twitter kwamba aliibuka mshindi kwa kupata kura 200.
Kuanzia wakati huo, wacheza filamu hao walikuwa wakitoa lugha za kukashifiana kupitia kwenye mitandao mbali mbali, hali iliyosababisha waonekane kuwa hawaelewani.
Baadhi ya wacheza filamu nyota wa Nollywood wamekuwa wakilalamikiwa kwa kukanusha taarifa zinazoripotiwa na vyombo vya habari juu yao, wakidai kuwa hazina ukweli, lakini baadaye hubainika kuwa ni za kweli.
Miezi kadhaa iliyopita, Ini aliripotiwa kuwa mja mzito, lakini alikanusha taarifa hizo kabla ya kukiri kwamba ni za kweli.
Mcheza filamu mwingine nyota, Uche Jombo naye aliripotiwa kufunga ndoa kwa siri Mei mwaka huu, lakini alikanusha taarifa hizo kabla ya kubainika baadaye kwamba zilikuwa za kweli.

No comments:

Post a Comment