KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, June 4, 2012

HIZI NDIZO JEZI MPYA ZA AZAM FC

Jezi mpya za Azam FC, ambazo zipo katika mchakato wa kutengenezwa, zimekuwa gumzo kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kama facebook, twitter na Blogs mbalimbali nchini.
Mashabiki wengi wa soka wameonekana kuvutiwa na jezi mpya huku wasambazaji wa bidhaa za nguo na baadhi ya maduka wakiomba muongozo wa namna ya kuzipata.
Kimsingi jezi hizi zipo katika mchakato wa kutengenezwa, kwa sasa tunasubiri sampo kutoka China na baada ya hapo tukiridhika nazo ndipo tutatoa oda na inaweza kuchukua hadi miezi miwili kwa jezi kuwa tayari, kwa hiyo mashabiki wasitarajie kwamba zitatoka mapema, amesema katibu mkuu wa Azam FC Nassor Idrissa
Azam FC imejijengea heshima kwa kuwa inatoa toleo jipya la jezi kila msimu, huu ukiwa ni msimu wake wa tatu, ambapo msimu uliopiza jezi hizo zilidhaminiwa na Azam Cola na msimu huu itakuwa Azam Energy Drink.

No comments:

Post a Comment