KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, June 22, 2012

Simba yapokewa kwa shangwe Mwanza

KIKOSI cha timu ya soka ya Simba kimewasili mjini Mwanza leo asubuhi kwa ziara ya mechi mbili za kirafiki katika mikoa ya kanda ya ziwa.

Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga amesema leo kuwa, timu hiyo ilipata mapokezi makubwa badaa ya kuwasili Mwanza kwa ndege ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATC).

Kamwaga alisema timu hiyo itacheza mechi yake ya kwanza kesho kwa kumenyana na Toto African kwenye Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza.

Kwa mujibu wa Kamwaga, mabingwa hao wa Tanzania Bara watacheza mechi ya pili Jumapili kwa kumenyana na Express ya Uganda kwenye uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.

No comments:

Post a Comment