KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, June 13, 2012

Kuziona Twiga Stars, Ethiopia buku mbili

Kiingilio cha chini kwa mechi ya kufuzu kwa fainali za Afrika kwa Wanawake (AWC) kati ya Tanzania (Twiga Stars) na Ethiopia itakayochezwa Jumamosi (Juni 17 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni sh. 2,000.

Kiwango hicho ni kwa washabiki kwa viti vya bluu, kijani na rangi ya chungwa. Viti hivyo kwa pamoja vinachukua jumla ya watazamaji 48,590 kwenye uwanja huo wenye uwezo wa kuchukua washabiki 60,000.

Viingilio vingine kwa mechi hiyo itakayoanza saa 10 kamili jioni ni sh. 5,000 kwa VIP B na C wakati VIP A itakuwa sh. 10,000. Tiketi zitauzwa uwanjani siku ya mechi kuanzia saa 3 asubuhi.

Mechi hiyo itachezeshwa na waamuzi Grace Msiska atakayepuliza filimbi wakati wasaidizi wake ni Bernadettar Kwimbira, Happiness Mbandambanda na Linda Chikuni, wote kutoka Malawi. Kamishna ambaye anatoka Kenya ni Maqulate Atieno. Waamuzi hao wanawasili leo.

WAAMUZI KOZI YA FIFA KUPIMWA UFAHAMU WA ALAMA

Waamuzi 54 wanaoshiriki kozi ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) iliyoanza Juni 11 mwaka huu, kesho (Juni 14 mwaka huu) watahamia Uwanja wa Karume kwa ajili ya mazoezi ya alama (signals). Mazoezi hayo yatafanyika kuanzia saa 1-4 asubuhi.

Kozi hiyo itakayomalizika kesho (Juni 14 mwaka huu) inaendeshwa na wakufunzi Carlos Henriques na Mark Mizengo kutoka FIFA wakisaidiwa na wakufunzi wengine wanne wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF). Wakufunzi wa TFF ni Kapteni mstaafu Stanley Lugenge, Leslie Liunda, Soud Abdi na Riziki Majala.

Waamuzi wanaoshiriki ni 14 wa Tanzania wenye beji za FIFA ambao ni Erasmo Jesse, Ferdinand Chacha, Hamis Changwalu, Hamis Maswa, Israel Mujuni, John Kanyenye, Josephat Bulali, Judith Gamba, Mwanahija Makame, Oden Mbaga, Ramadhan Ibada, Saada Tibabimale, Samuel Mpenzu na Sheha Waziri.

Washiriki wengine ni 20 wa daraja la kwanza (class one), kati ya hao watano wanatoka Zanzibar. Vilevile wapo waamuzi chipukizi (watoto) 20, ambao mwaka jana walitumika katika michuano ya Kombe la Uhai na Copa Coca-Cola.

No comments:

Post a Comment