KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, June 27, 2012

EUCHARIA: Bado natamani kuolewa

LAGOS, Nigeria
MIEZI michache baada ya kuamua kuokoka na kuwa mchungaji, mcheza filamu Eucharia Enunobi amesema bado anatamani kuwa na mume makini.
Eucharia, ambaye ni mama wa mtoto mmoja amesema amekuwa akimuomba Mungu kila kukicha ili aweze kupata mume mwema na makini.
Mwanadada huyo amesema hajawahi kuishi katika maisha matamu ya kimapenzi na anatamani siku moja aweze kuyapata maisha hayo.
“Sijawahi kuwa na maisha ya kimapenzi na mwanaume. Ninaposema maisha ya kimapenzi, simaanishi kwamba wanaume hawanitongozi. Watu wananitongoza, lakini kama ni kwa staili ya kitu kinachoitwa rafiki wa kiume, hapana,”alisema mwigizaji huyo aliyejizolea sifa na umaarufu kutokana na staili yake ya uigizaji. “Siwezi kufanya kitu kama hicho, lakini naomba kwa Mungu niwe na mwanaume, ambaye atakuwa mume wangu,”alisisitiza.
Eucharia alisema anaamini Mungu atamjalia kupata mume bora haraka iwezekanavyo, lakini alisisitiza kwamba, kwa sasa hilo halimsumbui kwa vile yupo bize katika kazi ya kuhubiri dini.
“Naelewa kuwa katika maisha kuna vishawishi vya hapa na pale. Hivyo napenda kusema kwamba katika siku si nyingi zijazo, rafiki yangu atajitokeza na upweke kwangu utatoweka, lakini sina wasiwasi kwa hilo,”alisema.
“Biblia inanifanya niwe bize kutokana na kuhubiri injili. Kutembea kunanifanya niwe bize. Naelewa na kutambua kwamba kila kitu kinakwenda kutokana na mipango ya Mungu. Naamini hivi karibuni atanikutanisha na mwanaume sahihi kwangu,”aliongeza.
Eucharia, ambaye amecheza filamu nyingi, ikiwemo Glamour Girls, hivi karibuni aliibuka na filamu yake ya kwanza, inayojulikana kwa jina la The Kingdom.

No comments:

Post a Comment