KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, June 25, 2012

Miss Universe Tanzania 2012 kusakwa Ijumaa

MASHINDANO ya kumsaka mrembo wa Miss Universe Tanzania 2012 litafanyika Ijumaa hii kwenye ukumbi wa Makumbusho ya Taifa yaliyopo Posta jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Compass Comm unications, Maria Sarungi Tsehai alisema jana kuwa mashindano hayo yatashirikisha jumla ya warembo 20 kutoka katika mikoa mbali mbali ya Tanzania Bara.

Aliitaja mikoa hiyo kuwa ni Manyara, Arusha, Dodoma, Mwanza, Mtwara, Kilimanjaro na wenyeji Dar es Salaam na kuongeza kwamba warembo wote wanaendelea na mazoezi chini ya wakufunzi walioboea katika masuala ya urembo.

“Tunatarajia kuwa na mashindano bora ili kuweza kumapata mrembo ambaye atatupa sifa katika mashindano ya kimataifa kama ilivyokuwa kwa Flaviana Matata mwaka 2007 ambapo alishika nafasi ya saba katika mashindano yaliyofanyika nchini Mexico,” alisema Maria.

Maria aliwataja warembo hao kuwa ni Bahati Chando, Aisha Maulidi, Catherine Mpulule, Cecilia Moses, Consolata Mosha, Devotha Keregese, Doris Mollel, Doreen Mapunda na Edith Tesha.

Wengine ni Getrude Asanterabi, Jescha Tiba, Kundi Mligwa, Lilian Kolimba, Mary Joel, Naomi Joseph, Nyaso Malilo, Neema Mpanda, Susan Manoko, Theodora Msenya na Winfrida Dominic.

Alisema kuwa shindano hilo limedhaminiwa na gazeti la The Citizen, gazeti dada la Mwananchi kwa kushirikiana na wadhamini wengine, Le Grand Casino, Urban Rose Hotel, Amina Design, Dodoma Hotel na New York Film Academy.

Maria alisema kuwa shindano hilo litaanza saa 1.00 usiku kwa warembo hao kupita jukwaani wakiwa katika aina mbalimbali za mavazi kama vile ya ubunifu na lile la usiku.

Alisema kuwa maandalizi kwa ajili ya shindano hilo kubwa la urembo yamekamilika na kinachosubiliwa ni siku ya shindano hili kupata mrithi wa Miss Universe anayemaliza muda wake Nelly Kamwelu.

Alifafanua kuwa wameboresha mashindano ya mwaka huu na wanatarajia kuwa na mashindano bora kabisa tofauti na ya miaka ya nyuma.

No comments:

Post a Comment