KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, June 28, 2012

VODACOM KUZIZAWADIA SIMBA, AZAM J'MOSI

Kampuni ya Vodacom itakabidhi zawadi kwa washindi wa Ligi Kuu ya Vodacom msimu 2011/2012 katika hafla itakayofanyika Juni 30 mwaka huu kwenye hoteli ya Double Tree Hilton jijini Dar es Salaam.
Hafla hiyo itakayohudhuriwa na wawakilishi wawili kutoka katika klabu za Ligi Kuu, itaanza saa 12 jioni.

Katika hafla hiyo, washindi mbalimbali wakiwemo bingwa, makamu bingwa na mshindi wa tatu watakabidhiwa zawadi zao.

Wengine watakaozawadiwa ni mfungaji bora, kipa bora, timu bora yenye nidhamu, mchezaji bora wa ligi, refa bora na kocha bora.

Mabingwa wa ligi hiyo msimu uliopita ni Simba, wakifuatiwa na Azam na Yanga. Mfungaji bora ni John Bocco wakati kipa bora ni Juma Kaseja.

No comments:

Post a Comment