KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, June 27, 2012

Mimi ni albino-Doris Simeon


LAGOS, Nigeria
MCHEZA filamu chipukizi wa Nollywood, Doris Simeon, ambaye ndoa yake ilikumbwa na misukosuko hivi karibuni, amefichua kuwa yeye ni albino.
Doris ameueleza mtandao wa naijerules hivi karibuni kuwa, watu wengi hawatambui kuhusu ukweli huo ndiyo sababu iliyomfanya aweke mambo hadharani. ‘Mnaelewa kwamba mimi ni albino na ni rahisi kunigundua kwa sababu ya mwonekano wangu. Hakuna njia, ambayo itamfanya albino asiweze kutambulika mbele ya kundi la watu,’ alisema.
Doris ni mtoto wa pili katika familia ya watoto watano wenye ulemavu wa ngozi ya mwili na asili yake ni Benin katika jimbo la Edo, lakini alizaliwa na kukulia katika jiji la Lagos.
Alipata elimu ya sekondari katika shule ya Maryland na baadaye katika chuo cha PEFTI. Amecheza filamu nyingi za Nollywood na kwa sababu ameanza kutengeneza filamu zake.
Hivi karibuni, Doris aliripotiwa akimlalamikia mcheza filamu mwenzake, Stella Damasus.

No comments:

Post a Comment